Tamasha la kuendesha baiskeli uchi, mwaka Huu litafanyika Agosti 26.
Tamasha hilo la kuendesha baiskeli uchi la Philly katika jimbo la Philadelphia la Marekani utafanyika Agosti 26.

Waendesha Baiskeli wakiwa uchi.
Waandalizi wa msafara huo wa kila mwaka ambao unalenga kukuza uhifadhi wa mafuta na taswira nzuri ya mwili waliambia vyombo vya habari vya Marekani siku ya Jumatano kwamba eneo la kuanzia na njia bado haijafungwa hadi siku moja kabla.
Kulingana na waandalizi wa tamasha hilo, safari hiyo ya kilomita 16 ni sehemu ya vuguvugu la kuendesha baiskeli uchi ulimwenguni na huvutia waendesha baiskeli wapatao 3,000.
Waandalizi wanasema wanatumai kuwa inawahimiza watu kuendesha baiskeli zaidi na kukumbatia uchi kama sehemu ya kawaida na ya kufurahisha maishani.
Hapo awali, safari hiyo ilifanyika mnamo Septemba lakini waendesha baiskeli hao waliokuwa uchi walisema ilikuwa baridi sana. Ilibadilishwa kufanyika kila Agosti mnamo 2019.