Afrika Wakawaka ni wimbo unaolizungumzia Bara la Afrika kwa jinsi lilivyobarikiwa kwa vivutio vingi, watu wenye upendo,jinsi tunavyouenzi utamadini wetu, ngoma zetu za asili, mavazi yetu ya asili na lugha zetu hasa Kiswahili kinavyosambaa kwa kasi Barani Afrika na Duniani.

”Nimeimba wimbo huu Afrika Wakawaka ili kuwakumbusha waafrika kuwa tunatakiwa tujivunie uafrika na vilivyomo Barani Afrika,” alisema Dinamite.
Karibu Kuusikiliza.